Advertise here

Tuesday, January 15, 2013

SKYLIGHT YAENDELEA KUWABAMBA MASHABIKI WA MUZIKI WA LIVE BAND JIJINI DAR

Mary Lukas katika hisia kali.....
Vijana wa SKYLIGHT BAND.... Rappa Sony Masamba sambamba na Joniko Flower taratibu katika miondoko ya Zouk Rhumba. Kikongo na Kizaire kimelala hapo.
I feel you Girls.....Shabiki anapokunwa na wimbo, hawezi kuvumilia.
Pichani Juu na Chini Sehemu ya Mashabiki wa SKYLIGHT BAND wakiserebuka kwa raha zao.
Vitu adimu kama hivi havikosekani...Wadada warembo wakishow love na pozi matata.
Kipaji kimelala hapo......Aneth Kushaba AK47 na Sony Masamba wakitoa burudani kwa mashabiki wa SKYLIGHT BAND katika kiota cha Thai Village Masaki mwishoni mwa Juma jijini Dar.
Sam Mapenzi, Sony Masamba na Joniko Flower wakiporomosha burudani ya aina yake kwa mashabiki wa SKYLIGHT BAND.
Couples ya Ukweli ndani ya nyumba.
Vijana watanashati hawakosekani.
Mdau King Kif akishow love na mshikaji wake.
Warembo katika pozi na kaka yao....Hatekwi mtu hapa.....

BEYONCE ALAANIWA KWA KUISHABIKIA SODA!

WAKATI wasanii wakubwa wa kimataifa wakiaminika kuwa kioo cha jamii na mfano bora wa kuigwa na watu wengi, kitendo cha msanii Beyonce Knoweles wa Marekani kukubali kuwa balozi wa kinywaji cha soda aina ya Pepsi, kimelaaniwa na kukosolewa na wakereketwa wa masuala ya afya!
Beyonce Knoweles.
Vyakula visivyo na virutubisho (Junk Food) pamoja na vinywaji vyenye kiwango kingi cha sukari ndivyo vinaaminika kuchangia kwa kiwango kikubwa ongezekao la magonjwa hatari ya kisukari, shinikizo la damu na hata kiharusi, na siyo kwa watu wazima tu, bali hata kwa watoto wadogo.
Kwa mujibu wa mwandishi mahiri wa masuala ya afya wa nchini Marekani, Dk. Mercola, makampuni makubwa duniani ya vyakula visivyo na lishe bora na makampuni ya vinywaji baridi, hutumia zaidi za dola za kimarekani bilioni 2 (zaidi shilingi trioni 3) ku promoti bidhaa zao hatari ili zitumiwe na watu wakiwemo watoto.
Ingawa jukumu la kuhakikisha mtoto anakula chakula na kunywa vinywaji bora kwa afya ya binadamu ni la mzazi, lakini kitendo cha makampuni hayo kutumia wasanii wakubwa kama Beyonce kwenye matangazo yao, kinaifanya kazi ya wazazi kutekeleza jukumu lao kuwa ngumu.
Wengi tunapenda kuiga, hasa watoto, vitu vinavyofanywa na watu maarufu, iwe kwenye chakula na hata muonekanao, hivyo staa kama Beyonce anapoonekana anatumia soda ya aina fulani, si rahisi kumkataza mtoto kuitumia soda hiyo, hawezi kukuelewa!
Hivi karibuni, mwanamuziki huyo ameingia mkataba mnono wa dola za Kimarekani milioni 50 (zaidi ya bilioni 80 za kibongo) ambazo atalipwa na kampuni ya Pepsi kwa kuwa balozi wake wa dunia wa kinywaji hicho.
Wakati huku kwetu kitu chochote kinachopitishwa na wasanii wa kimataifa kinaigwa kirahisi, hali ni tofauti kwa nchi kama Marekani. Kitendo cha Beyonce kusaini mkataba huo kimezua mjadala mkubwa kuona baadhi ya wanaojiita ‘mfano mzuri wa kuigwa’ (role models) hawafanyi kwa vitendo vitu wanavyopaswa kufanya ili kuwa mfano mzuri wa kuigwa na jamii.
Kufuatia taarifa hizo za Beyonce, mtandao wa frugivoremag.com umeandika maoni kadhaa ya kulaani kitendo hicho;
 “Wakati baadhi ya mashabiki wamefurahia mkataba wa Beyonce, wangine wamelaani kitendo cha kuunga mkono kinywaji chenye sukari ambacho kinachangia matatizo ya kiafya ya Wamarekani wengi hivi sasa.
“Wengine wamemtuhumu Beyonce kwa unafiki kwani upande mmoja ameonekana kuungana na kampeni ya Baraka Obama na mkewe Michelle ya kuwahimiza Wamarekani kujali afya bora za watoto, wakati upande mwingine anaunga mkono kinywaji ambacho kinachangia matatizo mengi ya kiafya ya watoto wa Kimarekani.
“Wakati magonjwa hatari kama Kutetemeka mwili (Parkinson’s Disease), magonjwa ya moyo, kiharusi na shinikizo la damu yakiwa yameshamiri duniani, wengine wanalipwa mamilioni ya dola ili kuimarisha magonjwa hayo,” aliandika pia mtoa maoni mmoja kwenye mtandao huo.
Utafiti uliyopo kuhusu unywaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi unaonesha kuwa matumizi yote ya vinywaji hivyo yana uhusiano mkubwa na hatari ya mtu kuongezeka uzito wa mwili na kuwa tipwatipwa, hali ambayo huongeza hatari ya kupatwa na magonjwa ya kisukari, shinikizo la juu la damu, na magonjwa ya moyo.
Aidha, kila kinywaji cha ziada chenye sukari anachotumia mtoto, huongeza uwezekano wa kuongezeka uzito na kuwa tipwatipwa kwa asilimia 60. Unywaji wa soda kila siku, unaongeza hatari kwa wanaume ya kupatwa na ugonjwa wa moyo kwa asilimia 19. Unywaji wa vinywaji viwili au kimoja vyenye sukari kwa siku, huongeza hatari ya mtu kupatwa na ugonjwa wa kisukari aina ya pili, kwa asilimia 25!
Kimsingi, makapuni ya vinywaji baridi yanatumia mabilioni ya pesa kila mwaka kutangaza biashara zao na kuzifanya zionekane hazina madhara kwa watumiaji, hivyo hatuna budi kuelewa na kukubaliana na ukweli kwamba vinywaji vyenye sukari, hata kama siyo pombe, ni hatari sana kwa afya zetu na watoto wetu wako hatarini zaidi.
Tunashauriwa tusiwazoeshe watoto wetu unywaji wa soda na vinywaji vingine vitamu na badala yake tuwazoeshe kunywa vinywaji halisi na visivyo na sukari, kama vile juisi za matunda halisi bila kuweka sukari, maji na vinywaji vingine kama hivyo. Kama huamini vinywaji baridi ni hatari, jiulize kwa nini hivi sasa hata watoto wadogo wanaugua ugonjwa wa kisukari na saratani?
Tafakari, chukua hatua!

Simba Full Muziki



Simba wakiwa kwenye mazoezi yao nchini Oman
DORIS MALIYAGA, OMAN
SIMBA sasa wapo kamili. Baada ya kutua kwa nyota wake waliokuwa Taifa Stars na Kombe la Mapinduzi Zanzibar kumekamilisha kikosi chake kilichopiga kambi hapa Muscat, Oman.

Wachezaji watatu Amir Maftah, Edward Christopher na Mussa Mudde ndio wachezaji ambao hawajajiunga na kambi ya Simba hapa Oman kutokana na sababu mbalimbali.

Meneja wa timu hiyo, Jamhuri Kihwelo alisema kila mmoja amebaki kutokana na sababu zake.

"Maftah amebaki kwa tatizo la nidhamu, Mudde amepata matatizo ya kifamilia yuko kwao Uganda."

Christopher, hata hivyo, amebakizwa baada ya kuumia kwenye mashindano ya Kombe la Mapinduzi.

Maftah alitakiwa kutua jana Jumatatu na wenzake waliokuwa Taifa Stars lakini alizuiwa kuondoka kutokana na utovu wa nidhamu, ambao haukuwekwa wazi na Julio.

Simba inajifua vilivyo tangu walipofika Januari 9, ingawa walifika kwa mafungu tofauti.

Walianza wakiwa na wachezaji nane, wakaongezeka kufikia 13 na sasa wametimia 24.

Nyota walioko Oman ni pamoja na Juma Kaseja, Ramadhani Chombo 'Redondo', Haruna Moshi, Boban', Mzambia Felix Sunzu, Said Nassor 'Cholo', Haruna Shamte, Haruna Chanongo, Kigi Makassy, Abdallah Seseme, Ramadhan Singano, Mrisho Ngassa na Mwinyi Kazimoto.

Wengine ni Abdallah Juma, Paul Ngalema, Amri Kiemba, Shomari Kapombe, Abel Dhaira na baadhi kutoka timu ya yosso ya Simba.

Kocha mkuu wa kikosi hicho, Mfaransa Patrick Liewig amesema lengo lake na tabia yake kama dereva ni kuhakikisha Simba inakuwa timu nzuri.

�Tunatakiwa kufanya kazi ili tufanikiwe ambapo sasa natengeneza timu ya ushindi tu.�

Viwanja tofauti
Simba inafanya mazoezi katika viwanja vitatu. Kuna siku inafanya kwenye uwanja wa klabu ya Fanja.

Mara nyingine wanajifua katika Uwanja wa Klabu ya Michezo inayoitwa Oman.

Simba pia imefanya mazoezi katika Uwanja wa Michezo wa Sultan Qaboos, ambao unamilikiwa na serikali ya hapa.

Total Football
Kocha Liewig amesisitiza kitu anachokifanya sasa ni kutengeneza timu yenye kushirikiana ambayo itashambulia pamoja na kuzuia pamoja lakini pia iwe inafunga mabao.

Staili hiyo kwa jina la kimombo huitwa `Total Football�, ambayo ilikuwa inachezwa zaidi na timu za Uholanzi kwenye miaka ya 1970.

Pengine hiyo ni janja ya Liewig kuanza kusuka mbinu za kuidhibiti Yanga, ambayo inanolewa na Mholanzi Ernest Brandt.

Kumbuka Brandt alikuwemo katika kikosi cha timu ya taifa Uholanzi kilichotikisa na staili hiyo chini ya kocha Rinus Michel.

�Muhimu ninachokifanya ni kutengeneza kombinesheni ya timu. Nilikuwa Zanzibar na nimeiona timu ikicheza nimegundua upungufu hasa katika ushambuliaji na kujihami.�

Nataka mambo yafanywe na timu kwa pamoja kwani yatasaidia kuongeza ushirikiano wa wachezaji na timu kuwa ngumu kufungika.

Sunzu, Kazimoto waugua
Sunzu alikatiza mazoezi ya jana Ijumaa jioni baada ya kufanya kwa nusu saa. Alikimbizwa hospitali na aligundulika alikuwa na tatizo la kifua.

Hata hivyo, kitendo hicho cha kukatiza mazoezi na kulalamika kujisikia vibaya kuliwatia hofu watu pengine tatizo lake la moyo lilikuwa limerudi.

Sunzu alitaka kukatiza mkataba na Simba kwenye Dirisha Dogo la usajili kwa madai alikuwa ana tatizo la moyo.

Ingawa baada ya muda alibadili mawazo na kurudi nchini na kujiunga na Simba tena.

Kipa Dhaira naye alipelekwa hospitali baada ya kufanya mazoezi ya asubuhi. Pia naye alikuwa na tatizo la kifua na alipewa dawa.

Kazimoto hakufanya kabisa mazoezi na aligundulika alikuwa na malaria.

Sunzu na Boban
Liewig anaeleza kuwa anataka Sunzu na Boban ndio waongoze safu ya ushambuliaji.

�Nimeanza na hawa kwa kuwa ndio nilikuwa nao kwa kipindi chote kwa sasa wamekuja hawa wengine mambo yatakuwa mazuri zaidi naweza kuamua namna gani nitakavyowachezesha,� alieleza Liewig.

Mfaransa huyo anaona nyota hao wawili wanaweza kutengeneza safu kali ya ushambuliaji.

Kocha huyo amefurahia ujio wa wachezaji wote lakini amesisitiza muda wa siku 10 uliobaki ni mfupi kwa maandalizi yake.

Simba walikiwa na idadi kubwa ya wachezaji walifanya mazoezi jana Jumatatu katika Uwanja wa Oman na walianza kwa mazoezi ya kukimbia chini ya Julio.

Katika mazoezi hayo walifanya ya ufundi kwa kucheza pasi ndefu na fupi ambapo kocha amesisitiza lengo ni umakini kwa
mchezaji anapokuwa na mpira kwa kutoa pasi na kupokea.