Baada
ya kufanyiwa majaribio asubuhi ya leo Xavi Hernandez imegundulika
kwamba atakuwa nje kwa takribani siku 15 na atakosa mechi mbili zijazo
kati ya Getafe na Granada, Ingawa kupona kwake kunaenda kama
ilivyopangwa, Xavi atarudi uwanjani wakati michezo ya Champion League
wakicheza na Milan mechi itakayochezwa tarehe 20 mwezi 20. Xavi pia
atakosa pia mechi kati ya kirafiki dhidi ya Uruguay Jumatano. Xavi
amecheza mara 33 msimu huu na amefunga magoli 6, Xavi alicheza karibia
mechi yote Jumapili pale Mestalla na alitoka na kubadilishana na Thiago
katika muda wa nyongeza.
Monday, February 04, 2013
MADUKA YATEKETEA KWA MOTO MWENGE
Hivi
ndivyo eneo la Mwenge kituoni lilivyokuwa majira ya saa tano asubuhi
ambapo shughuli zote ikiwemo usafiri wa Daladala kuelekea katikati ya
Jiji na maeneo mengine zilisimama ili kupisha vikosi vya Zima Moto na
Uokoaji vya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuzima moto uliokuwa
ukiteketeza baadhi ya maduka.
Licha ya Moto huo kuonesha kuwa na madhara zaidi, vikosi vya zimamoto vikishirikiana na vile vya Kampuni binafsi za Ulinzi vilifanikiwa kuuzima moto huo na kupunguza hatari ya kuhamia kwenye maduka mengine ambayo yamekaribiana.
Licha ya Moto huo kuonesha kuwa na madhara zaidi, vikosi vya zimamoto vikishirikiana na vile vya Kampuni binafsi za Ulinzi vilifanikiwa kuuzima moto huo na kupunguza hatari ya kuhamia kwenye maduka mengine ambayo yamekaribiana.
Akizungumzia
tukio, Mkuu wa Ulinzi Shirikishi Kituo cha Mabasi Mwenge KESSY MLUGURU
amesema, waligundua kutokea kwa moto huo katika moja ya duka majira ya
saa tatu asubuhi na kuanza juhudi za kuuzima kwa maji yakiyo kwenye
tenki ambapo Mkuu wa Kituo cha Polisi Mabatini Kijitonyama anathibitisha
kutokea kwa moto huo.
Mmoja ya Wamiliki wa maduka ya vipodozi ambayo yameteketea MAPINDUZI WILSON amesema, moto huo umetokea kutokana na hitilafu ya umeme iliyotokea kwenye moja ya waya zinazoingia kwenye maduka hayo.
Kwa upande wake Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam, Meja KURWA NZELEKELA amesema kikosi chake kinakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo miundombinu ya barabarani na usalama wanapokuwa kazini.
Tukio hili linafuatiwa na lile lililotokea jana kwenye Jengo la PPF TOWER lililopo Makutano ya Mtaa wa Ohio na Garden kunusurika kuteketea kwa moto baada ya moja ya ghorofa zake kushika moto ambao pia ulidhibitiwa na vikosi hivyo vya zima moto.
Mmoja ya Wamiliki wa maduka ya vipodozi ambayo yameteketea MAPINDUZI WILSON amesema, moto huo umetokea kutokana na hitilafu ya umeme iliyotokea kwenye moja ya waya zinazoingia kwenye maduka hayo.
Kwa upande wake Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam, Meja KURWA NZELEKELA amesema kikosi chake kinakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo miundombinu ya barabarani na usalama wanapokuwa kazini.
Tukio hili linafuatiwa na lile lililotokea jana kwenye Jengo la PPF TOWER lililopo Makutano ya Mtaa wa Ohio na Garden kunusurika kuteketea kwa moto baada ya moja ya ghorofa zake kushika moto ambao pia ulidhibitiwa na vikosi hivyo vya zima moto.
TUME YA KUKUSANYA NA KURATIBU MAONI YA KATIBA YAMALIZA HATUA ZA MSINGI
Tume
ya kukusanya na kuratibu Maoni ya Katiba nchini imesema imemaliza hatua
ya msingi ya kukusanya na kuratibu maoni kutoka kwa makundi maalum na
kubainisha kuwa hatua inayofuata sasa ni kuanza kwa zoezi la uchambuzi
wa maoni yote yaliyokusanywa pamoja na uandishi wa rasimu ya katiba
mpya.
Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu JOSEPH WARIOBA amesema kuwa uchambuzi huo unatarajiwa kufanywa na mabaraza maalum ya Katiba kuanzia June Mwaka huu, na kuongeza kuwa mabaraza hayo yatapatikana kupitia mapendekezo maalum kutoka kwa wajumbe wa Tume hiyo.
Akizungumzia uteuzi wa mabaraza hayo JAJI WAROBA amesema, tume hiyo imejipanga kuhakikisha watu watakaopatikana kuunda mabaraza hayo wanakuwa makini, na ambao watasimamia zoezi hilo haraka na kwa umakini zaidi ili kupata katiba itakayokuwa na tija kwa Watanzania.
Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu JOSEPH WARIOBA amesema kuwa uchambuzi huo unatarajiwa kufanywa na mabaraza maalum ya Katiba kuanzia June Mwaka huu, na kuongeza kuwa mabaraza hayo yatapatikana kupitia mapendekezo maalum kutoka kwa wajumbe wa Tume hiyo.
Akizungumzia uteuzi wa mabaraza hayo JAJI WAROBA amesema, tume hiyo imejipanga kuhakikisha watu watakaopatikana kuunda mabaraza hayo wanakuwa makini, na ambao watasimamia zoezi hilo haraka na kwa umakini zaidi ili kupata katiba itakayokuwa na tija kwa Watanzania.
LEO KATIKA ITV HABARI
Subscribe to:
Posts (Atom)