Kajala
ametoka kukumbana na kashikashi katika maisha yake hivi karibuni,
baada ya kusota jela takriban mwaka mmoja kutokana na kesi ya
kutakatisha fedha iliyomwandama yeye na mumewe ambaye yuko jela.
Akizungumza
katika kipindi cha ‘Take One’ kinachorushwa kila Jumanne na Clouds Tv,
Kajala alisema alipokuwa jela alimkumbuka mama yake kwa mambo
aliyokuwa akimwambia na kuanza kujuta kutokana na mateso aliyokutana
nayo huko.
“Mimi nilianza kumkumbuka sana mama yangu alivyokuwa akiniusia
kutulia, ila mimi natoroka nyumbani nakwenda ninakotaka na kumuacha
katika huzuni, ila nilipokaa jela niliona nini umuhimu wa mama, namuomba
anisamehe sikujua nilitendalo,” alisema Kajala
Aidha,
Kajala alisema katika familia yao, mama yake alikuwa ni mkali kuzidi
baba yake, ambaye kila kitu walichotaka kufanya aliwaruhusu, ikiwa ni
pamoja na kwenda katika majumba ya muziki, lakini mama yao alikataa na
kudai sasa anatambua umuhimu wake.
Aliwashukuru wote ambao walikuwa naye bega kwa bega hadi kufanikisha
kutoka jela, huku shukrani za pekee akizimwaga kwa msanii mwenzake Wema
Sepetu ambaye alimnusuru kufungwa jela miaka saba kwa kumlipia faini ya
sh milioni 13.
No comments:
Post a Comment