Advertise here

Tuesday, February 12, 2013

DIMPOZY ALIPOZINDUA KIOO CHA ME & YOU

Ommy Dimpoz na Vanessa Mdee baada ya kwenda Nairobi kwa ajili ya utengenezaji wa video yao mpya 'Me n You' chini ya production ya Ogopa video. Sasa usiku wa kuamkia leo Ommy Dimpoz alikuwa akiizindua rasmi video yake mpya kwa mashabiki wake.Huku wakisindikizwa na Mwana FA,Dully sykes,Diamond Platinum.
Hizi ni baadhi ya picha za maisha club katika uzinduzi huo wa video mpya Me n You.
Mtangazaji wa Clouds Tv Ciezer Daniel (KULIA) akiwajibika wakati wa shoo ya uzinduzi wa kichupa cha ngoma me&u cha Ommy Dimpoz ndani ya club Maisha. hapa alikuwa akimuhoji staa wa wimbo huo Ommy Dimpoz

DIMPOZY NA VANESSA WAKITENGENEZA ME & YOU CHINI YA OGOPA VIDEO'Z








KAULI YA PAPA KUHUSU KUJIUZURU KWAKE


Jana  kupitia vyombo mbalimbali  vya habari ulimwenguni ilitoka taaraifa kuhusiana na Kiongozi mkuu wa kanisa katoliki duniani Pope Bennedict  kutangaza kujiuzuru nafasi hiyo kwa kile kilichotangwazwa kuwa  umri wake kuwa mkubwa hivyo kushindwa kuhimiri  kasi ya baadhi ya majukumu yake.

SPIKA ANNA MAKINDA ATUKANWA KWENYE SIMU

Siku moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutangaza namba za Spika wa Bunge, Anne Makinda na Naibu wake, Job Ndugai, katika mkutano wa hadhara jijini Dar es Salaam, baadhi ya watu wamezitumia kumtukana Makinda. Chanzo kilichopo karibu na Spika kimesema kuwa tangu chama hicho kilipotangaza namba hizo za simu, jumla ya simu 200 za kumtukana Spika zilipigwa.

Hali kadhalika, katika kipindi hicho jumla ya ujumbe 400 mfupi wa simu za mkononi (sms), uliokuwa ukimtukana ulipokelewa katika simu zake.
“Simu hizo walikuwa wameshika wasaidizi wake, kila aliyepiga simu kwa lengo la kutukana, amekuwa akiachwa kutukana hadi anapomaliza na kisha kuambiwa sawa,” kilisema chanzo hicho ambacho hakikutaka jina lake liandikwe gazetini.

KAULI YA SITTA
Alipoulizwa kuhusiana na kutukanwa kwa Spika Makinda, Spika Mstaafu, Samuel Sitta, alisema kumtukana mtu mzima si maadili mema na kwamba hata kama kuna mambo ambayo mbunge hakubaliani nayo, nchi zote zimeweka taratibu za kushughulikia mambo kama hayo.
“Wanatakiwa kuwa wavumilivu…wafuate taratibu ambazo zimewekwa katika kushughulikia mambo hayo,” alisema.
Alisema amesikia kuwa wabunge wa Chadema wakirejea bungeni wameandaa mpango wa kusimama na kupiga kelele wakati kikao cha Bunge kikiendelea.
“Najiuliza ni mpango gani kama kupiga kelele, nimesikishwa sana mimi kama mtu mzima na mambo haya,” alisema Sitta ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Kwa upande wake, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema mambo yanayofanywa na Chadema ni dalili za kufilisika kisiasa.
“Bunge limeweka taratibu za kushughulika na rufaa na mambo ambayo upande mmoja unapinga, wao Chadema ndiyo kambi rasmi bungeni wanatakiwa kama kuna kitu wanakipinga kufuata taratibu zinazokubalika,” alisema.
Aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Tisa kupitia Jimbo la Iramba Magharibi (CCM), Juma Kilimbah, alisema siyo vibaya kutolewa kwa namba ya simu ya kiongozi, lakini kama kukiwa na dhamira nzuri.
“Nawatahadharisha waliopewa wasije wakachuuzwa wakamtukana Spika, maana hii inaweza kuwasababishia kuwa na kosa la jinai kwa kuwatukana watu,” alisema Kilimbah, ambaye kwa sasa ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM.
Kwa mujibu wa viongozi wa Chadema, lengo la kugawa namba hizo za simu ni kuwataka wananchi ambao waliwaita kuwa ni ‘mahakama ya umma’ wawatumie ujumbe mfupi wa simu za mkononi wa kuwataka Makinda na Ndugai wajiuzulu kutokana na kushindwa kuliendesha Bunge kwa kupendelea CCM na kuuonea upinzani.
Chadema wanadai kuwa kiti cha spika kimekalia rufani za miongozo mingi bila kuitolea majibu tangu mwaka 2011.
Miongoni mwa ushahidi wa miongozo na rufaa zilizowasilishwa katika ofisi ya Spika ni ya kiti kwa kukataa kuliwezesha Bunge kujadili hali ya huduma katika hospitali za umma na jaribio la kutaka kuuawa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka uliotolewa na Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika.
Nyingine ni kutoridhishwa na uamuzi wa Naibu Spika wa kukataa mgomo wa walimu na yatokanayo na mgomo huo kujadiliwa bungeni, malalamiko dhidi ya uamuzi wa Mwenyekiti wa Bunge, Jenista Muhagama, kwa kudai kuwa Mnyika anao ushahidi kuwa Mbunge wa Iramba Magharibi, Lameck Mwigulu Nchemba (CCM), ni mmoja wa watuhumiwa wa kesi za Epa na kumtaka kuwasilisha ushahidi.
Uamuzi kuhusiana na uthibitisho kuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), juu ya kauli ya uwongo unaodaiwa kutolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, bungeni wakati akijibu maswali Februari 10, mwaka 2011.
Maamuzi mengine yanayodaiwa kutotolewa uamuzi na Spika, ni kauli ya Mbunge wa Meatu (Chadema), Meshack Opulukwa, ambaye alisema bungeni kuwa Mkuu wa wilaya hiyo, Abihudi Saideya, alihongwa gari ili ampatie mwekezaji kitalu cha uwindaji kwenye pori la akiba ili wananchi waondolewe eneo hilo.
Uamuzi mwingine ambao haujatolewa ni wa Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya (CUF), ambaye alitakiwa kuwasilisha uthibitisho wa kauli yake kuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo, aliingia katika zizi la mfugaji na kutoa mbuzi kisha kumchinja bila ridhaa ya mmiliki.
Uamuzi mwingine ni mwongozo wa kuhusu kauli ya Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, ambaye alisema kuwa majaji wengi wanateuliwa bila kuwa na sifa.
Mwongozo mwingine ambao haujatolewa maamuzi licha ya kuwasilishwa kwa ushahidi, ni Baraza la Mawaziri kushawishi Shirika Hodhi la Mashirika ya umma (CHC) lisiongezewe mkataba.
Viongozi wa Chadema waligawa namba za viongozi hao wa juu wa Bunge Jumapili iliyopita katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Temeke Mwisho, jijini Dar es Salaam.
NDUGAI AWAJIBU CHADEMA
Kufuatia shinikizo hilo, Ndugai amesema kuwa Chadema wanapaswa kufuata kanuni na sheria zilizomo katika katiba za kuwaondoa madarakani viongozi kuliko kutumia njia ya maandamano.
Akuzungumza  jana kwa njia ya simu kuhusiana na alivyopokea wito wa Chadema wa kumtaka aachie ngazi, Ndugai alisema kuna sheria na taratibu zilizowekwa katika kuiongoza nchi, hivyo kila mtu anapaswa kuzifuata.
Alisema endapo Mbunge akimtaka rais, waziri, spika au kiongozi yeyote aliyeko serikalini kujiuzulu, inampasa kufuata utaratibu uliowekwa na siyo kutumia njia ya maandamano.
Ndugai alisema mbunge pia anaweza kuandika barua au kuwasilisha hoja bungeni ya kumtaka spika au naibu spika ajiuzulu na hoja hiyo itajadiliwa na wabunge.
“Wanapaswa kuwasilisha hoja bungeni, hoja itapokelewa lakini, siyo kwa njia ya maandamano, ile ni ofisi ya umma siyo yangu, kila mtu ana haki ya kuliongoza Bunge,” alisema Ndugai, ambaye alilalamikiwa na upinzani kwa hatua yake ya kukubali Bunge liondoe hoja ya Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi) kuhusu kasoro katika mtaala wakati wa Mkutano wa 10 uliomalizika wiki iliyopita

MWAKYEMBE ATIBUA HALI YA HEWA MOROGORO


WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amesema kuwa atasitisha mikataba yote ya magari yanayohusika kubeba mafuta na kusambaza katika Shirika la Reli Tanzania (TRL) kutokana na hasara inayopatikana badala yake kutumia usafiri wa shirika hilo.
Mwakyembe alisema hayo mjini Morogoro alipofanya ziara ya kushtukiza kwenye stesheni ya reli iliyopo mjini Morogoro na kudai kuwa hatakuwa tayari kuendelea kufumbia macho suala hili la usafirishaji wa mafuta kwa magari wakati shirika hilo lina uwezo wa kusafirisha mafuta kwa kutumia usafiri wao.
Alisema endapo shirika litatumia mabehewa yake kusafirishia mafuta shirika halitapata hasara kama inayoendelea kupata kutokana na kutumia magari binafsi kusambaza mafuta kwenye stesheni zote nchini. Kwa upande wa wafanyakazi wa shirika hilo Kituo cha Morogoro, Taferi Dimisheni na Ramadhani Dalueshi, walisema kuwa wanafanya kazi katika mazingira magumu licha ya kuwa taifa linategemea pato kupitia shirika hilo.
Walisema kumekuwa na tatizo la mabehewa ya mizigo kukaa muda mrefu kituoni hapo kutokana na kukosekana kwa mafuta katika kituo hicho.
“Inafikia wakati mafundi injini wanashindwa kutengeneza injini za treni kutokana na kukosekana kwa mafuta na kusababisha msongamano wa mabehewa ambayo yana mizigo ya wateja wao,” alisema Taferi
Kwa upande wake, dereva wa treni inayofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Morogoro, Rango Mboma alisema kuwa madereva wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu hali inayowasababisha kuwa na madeni mengi kutokana na kutegemewa na familia zao.
Alisema kuwa kipato wanachopata wao hata dereva wa boda oda wanawazidi kwa kipato hivyo Serikali inatakiwa kuwaboreshea masilahi wafanyakazi wa kituo hicho.
Akitoa ufafanuzi wa madai hayo Meneja wa Karakana ya Morogoro, Mhandisi Nejo Ngosomwile alikiri kuwapo kwa matatizo hayo likiwamo la mafuta.
hivyo kusababisha mabehewa ya mizigo kukaa kwa muda mrefu. Hivyo aliiomba Serikali kuboresha masilahi ya wafanyakazi wakiwamo madereva kwani wao ndiyo wanaotegemewa katika kusafirisha abiria.

WAZIRI WA ELIMU ATOA KAULI TATA KUHUSU MITIHANI YA KIDATO CHA SITA

Katika hali ya kushangaza na kusikitisha, naibu waziri wa elimu katika serikali ya JK ametoa mpya ya kufungua mwaka baada ya kuulizwa juu ya maendeleo ya mitihani ya kidato cha sita inayoendelea hivi sasa . Alipoulizwa na kituo cha EATV kupitia kipindi cha HOTMIX, waziri huyo mwenye historia ya kutofahamu vyema historia ya nchi yake alitoa jibu kuwa.....
 
"Sina taarifa yoyote kuhusiana na kuanza kwa mitihani ya kidato cha sita, kwasasa nipo kwenye kikao cha NEC, labda waulizeni waliopo DSM ofisini. Alipoulizwa zaidi aliendelea kusema mimi sijui kuhsuiana na mitihani ya kidato cha sita. Huyu ndie Naibu waziri wa elimu ndugu Mulugo."

CCM YATANGAZA WAJUMBE WAJUMBE 14 WA KAMATI KUU YA CCM

Breaking News: Halmashauri kuu ya CCM(NEC)imewachagua na kuwatangaza wajumbe 14 wa kamati kuu(CC),saba toka Bara na saba toka ZNZ.Baadhi yao ni Steven Wassira,Dk.Anna Tibaijuka,Dk.Hussein Mwinyi na Dk.Salim Ahmed Salim.

DJ CHOKA AWAFUNGUKIA WADAU KWA FACEBOOK

NINANUKUU
"NAOMBA NISEME KITU KIMOJA KWA NYIE MNAOFUNGUA PAGE ZA FACEBOOK NAKUWEKA MAMBO YENU MACHAFU NA YAKISHENZI KWENYE HIZO PAGE HALAFU MWISHO WA SIKU UNAMUWEKA DEMU YOYOTE KWA PAGE NA KUTOA NAMBA YA SIMU ISIYO SAHIHI ILI WATU TU WATUMIE MUDA HUO KUMTAFUTA HUYO DEMU."

HAKUISHIA HAPO ALIENDELEA KUTELEMSHA MISTARI YENYE HISIA KALI

"SASA HII PAGE LEO IMEWEKA PICHA YA DEMU NA KUWEKA NAMBA YANGU YA SIMU SIJUI MLIKUWA MNATAKAJE KWA MFANO MAZ#F#K#(ZIMEFICHWA KWA SABABU YA MAADILI)  NYIE. NAPIGIWA SIMU NA KUTUMIWA MSG WAKIZANI HUYO DEMU NDIO NAMBA YAKE SASA KAMA MMETUMWA KUFANYA HIVYO USHINDWE NA ULEGE MAZ#F#K# WAKUBWA NYIE TENA MAZ#F#K# KILA MKIHEMA NI M#Z#F#K#"
KAFUNGUKA KIHIVYO BABA NA NANIIIII
NAOMBA NISEME KITU KIMOJA KWA NYIE MNAOFUNGUA PAGE ZA FACEBOOK NAKUWEKA MAMBO YENU MACHAFU NA YAKISHENZI KWENYE HIZO PAGE HALAFU MWISHO WA SIKU UNAMUWEKA DEMU YOYOTE KWA PAGE NA KUTOA NAMBA YA SIMU ISIYO SAHIHI ILI WATU TU WATUMIE MUDA HUO KUMTAFUTA HUYO DEMU.

SASA HII PAGE LEO IMEWEKA PICHA YA DEMU NA KUWEKA NAMBA YANGU YA SIMU SIJUI MLIKUWA MNATAKAJE KWA MFANO MAZAFAKA NYIE. NAPIGIWA SIMU NA KUTUMIWA MSG WAKIZANI HUYO DEMU NDIO NAMBA YAKE SASA KAMA MMETUMWA KUFANYA HIVYO USHINDWE NA ULEGE MAZAFAKA WAKUBWA NYIE TENA MAZAFAKA KILA MKIHEMA NI MAZAFAKA

NDEGE YAMUUA MKUU WA MAJESHI GUINEA


Mkuu wa jeshi la Guinea, ameuawa kwenye ajali ya ndege katika nchi jirani ya Liberia, akiwa na maafisa wegine watano.
Generali Souleymane Kelefa Diallom, alikuwa anaongoza wajumbe wa Guinea, katika sherehe za kila mwaka za kuadhimisha siku ya kitaifa ya jeshi la Liberia.
Waliarifiwa kuwa hapakuwa na manusura wa ajali hiyo lakini haikufahamika mara moja idadi ya watu waliokuwa kwenye ndege hiyo.
Baadhi walisema kuwa ni wanajeshi 18 waliokuwa wameabiri ndege hiyo.
Kwa mujibu wa waziri wa habari ,ndege yenyewe ilianguka mjini Charlesville, karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Liberia.
Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirlief, alizuru eneo la ajali, Kusini mwa Monrovia.
Kulingana na shirika la habari la AP, kifo cha Jenerali Diallo, kilitangazwa na rais wa Guinea.
Rais alielezea kusikitishwa na habari za kifo hicho, alipokuwa anakitangaza.

WANAJESHI WA MALI WAENDELEZA MSAKO MKALI HUKO GAO

Gao
Wanajeshi wa Mali wanafanya msako wa nyumba hadi nyumba kufuatia makabiliano makali na makundi ya wapiganaji wa kiisilamu katika mji wa Gao Jumapili.
Mapigano baina ya wanajeshi wa serikali ya Mali na wapiganaji wa Kiislamu kwa mara ya kwanza yamefika kati-kati ya mji wa Gao, mji mkubwa kabisa kaskazini mwa nchi.
Mwandishi wa BBC aliyeko huko anasema wanajeshi wa Ufaransa wanatumia mizinga dhidi ya wapiganaji hao walioingia hapo kabla.
Anasema ghasia zilianza karibu na makao makuu ya polisi, lakini mapigano yametapakaa. Inaarifiwa baadhi ya wapiganaji wamejificha miongoni mwa wananchi.
Wanajeshi wa Ufaransa na Mali waliukomboa mji huo mwezi uliopita.
Shirika la habari la Ufaransa linaeleza kuwa wapiganaji wa Kiislamu waliovaa nguo nyeusi, huku wamebeba bunduki, waliteka eneo la kati ya mji wa Gao, mji wenye wakaazi wengi kabisa kaskazini mwa Mali.
Wapiganaji hao walipambana na wanajeshi wa Mali leo jioni kwa zaidi ya saa mbili na walionekana wakiranda mitaani kwa pikipiki na wengine walikuwa juu ya mapaa karibu na makao makuu ya polisi.
Karibu na makao hayo wanajeshi wa Mali walitumia makombora na kupambana kwa risasi na washambuliaji ambao wanafikiriwa kuwa wafuasi wa kundi la MUJAO, linalodai kupigana jihadi Afrika Magharibi.
Sauti zilizosikika ni risasi na mbuzi wakikimbia huku wakaazi wa mji wamejificha majumbwani mwao.
Tangu wanajeshi wa Ufaransa kuukomboa mji wa Gao, wapiganaji wa Kiislamu walipambana na wanajeshi nje ya mji lakini hii ndio mara ya kwanza wamefanikiwa kuingia ndani ya mji.

PAPA BENEDICT ATANGAZA KUJIUZURU

Huko Ujerumani, msemaji wa serikali amesema kuwa anaheshimu kazi kubwa iliyofanywa na Papa huyu aliyezaliwa katika Jimbo la Bavaria la nchini humo.
Papa Benedict
Baba Mtakatifu ameelezea kwamba matatizo ya kiafya yamemfanya kutangaza kujiuzulu

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron, amemsifu Papa kwa jitihada zake za kuimarisha mahusiano baina ya Vatican na Uingereza.
Askofu mkuu wa Canterbury amesema amazipokea taarifa za kujiuzulu kwa Papa kwa huzuni mkubwa ingawa anaelewa undani wa hatua yake.
Kiongozi wa Ujeremani, Bi. Angela Merkel amesifu mchango wa Papa wa kupendekeza mjadala baina ya makanisa, waislamu na wayahudi.
Alikumbusha hotuba ya Papa alipozuru bunge la Ujerumani mnamo mwaka 2011.
Uwamuzi na hatua ya Papa Benedict XVI wa kujiuzulu mwishoni mwa mwezi huu baada ya takriban miaka minane akiongoza Kanisa Katoliki kwa hoja kuwa umri wake wa miaka 85 ni mkubwa kiasi kwamba hawezi kuendelea kuhudumu zaidi ya umri huo.
Makao makuu ya Kanisa Katoliki huko Vatican yanasema yanatarajia Papa mpya atachaguliwa kabla ya mwisho wa mwezi wa tatu, na sherehe za Pasaka.
Tabia ya kujiuzulu kwa Papa si ngeni, ingawa ni tukio jipya katika karne za hivi karibuni.
Mwandishi wa BBC mjini Roma Alan Johnston anasema habari hizi zimetokea kama radi, na kwamba hakukua natetesi yoyote juu ya uwezekano kama huu.
Msemaji wa Vatikani Father Federico Lombardi, amesema kuwa hata wasaidizi wa Papa wa karibu mno hawakuwa na fununu juu ya tukio hili.
Kakake Papa huyu mzaliwa wa Ujerumani alipewa ushauri na Daktari wake asifanye ziara nyingine yoyote ya Marekani na kwamba kwa miezi kadhaa Mtakatifu Papa amekuwa akitafakari kujiuzulu.
Akizungumza kutoka nyumbani kwake huko Regensburg, Ujerumani, Georg Ratzinger amesema kuwa Kaka yake alikuwa ameanza kupata shida ya kutembea na kwamba kujiuzulu kwake ni hatua ya kimaumbile.
Wakati wa kutawazwa kama Papa, Kadinali Joseph Ratzinger alikuwa mmojawapo wa mapapa wapya kuchaliwa akiwa mwenye umri mkubwa wa miaka 78.
Alitangazwa Papa mnamo mwezi Aprili 2005 kufuatia kifo cha marehemu John Paul wa pili.
Uongozi wake ulitokea wakati wa wimbi kali la ubakaji kulikumba kanisa katoliki katika kipindi cha miongo mingi, ubakaji uliofanywa na watawa dhidi ya watoto wavulana.
Katika taarifa yake, Mtakatifu Papa amesema: "baada ya kujichunguza binafsi na nafsi yangu mbele ya Mola wangu, nimefikia uwamuzi kua uwezo wangu na afya, ukiambatana na umri mkubwa, ni mambo yatakayokwaza jitihada zangu za kuendelea kuliongoza Kanisa Katoliki.
Kuna kipengele katika sheria ya Kanisa kinachosema kuwa kujiuzulu kwa Papa kunakubalika iwapo kitendo hicho kimefanywa kwa hiari na kwa utaratibu unaostahiki.