Maoni ya Annan yaliibua mjadala mkubwa kutoka kwa Wakenya wengine wakamchukia
Nairobi. Kundi muhimu ambalo
lilisaidia kwa karibu kuunda Serikali ya Kenya ambalo lilikuwa
likiongozwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan
halikuweza kuhudhuria kuapishwa kwa Rais Uhuru Kenyatta.
Taarifa kutoka Kenya zilisema kwamba Kofi Annan
ambaye aliongoza kuundwa kwa Serikali ya Muungano baada ya Uchaguzi Mkuu
wa 2007 hakuweza kuonekana katika sherehe hizo.
Pia waliokosekana ni wanachama wa kundi la Dk Annan ambao ni pamoja na Graca Machel na Benjamin Mkapa. Kundi hilo ndilo lilisaidia kuunda Serikali hiyo.
Pia waliokosekana ni wanachama wa kundi la Dk Annan ambao ni pamoja na Graca Machel na Benjamin Mkapa. Kundi hilo ndilo lilisaidia kuunda Serikali hiyo.
Lakini muda mfupi kabla ya Uchaguzi Mkuu, Annan alitaka uchaguzi nchini ufanyike kwa amani.
Mwaka jana , Annan aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja
wa Mataifa alizua malumbano alipowahimiza Wakenya wasiwachague
wanasiasa walioshtakiwa na Mahakama ya Kimataifa Kuhusu Uhalifu (ICC).
Ingawaje hakuwataja Rais Kenyatta na Naibu wake
William Ruto, wanaokabiliwa na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu
katika mahakama hiyo iliyopo The Hague, Uholanzi, Annan aliliambia
shirika la BBC kuwa kuwachagua viongozi wa aina hiyo kutaathiri uhusiano
wa Kenya na jamii ya kimataifa.
Maoni yake yaliibua majibu kutoka kwa wafuasi wa
chama cha Rais Kenyatta cha The National Alliance (TNA) na wa United
Republican Party (URP) cha Ruto.
No comments:
Post a Comment