Rais mpya wa Kenya, Uhuru Kenyatta ametangaza kumalizika kwa
muda wa Serikali ya muungano iliyopita, hivyo kufungua njia ya uteuzi wa
Baraza Jipya la Mawaziri litakaloongoza Serikali yake.
Hatua ya Kenyatta inamaanisha kumaliza zama za
utawalka wa Rais Mwai Kibaki aliyemaliza muda wake, baada ya uchaguzi
uliofanyika Machi 4 na kumpa ushindi Kenyatta pamoja na mgombea mwenza
wake, William Ruto.
“Kwa mujibu wa Katiba Mpya ya Kenya iliyopitishwa
mwkaa 2010, Serikali iliyokuwa ikiongozwa na Rais Mwai Kibaki ilimaliza
muda wake usiku wa Aprili 9,” alieleza Kenyatta katika taarifa yake
iliyosambazwa na Ikulu ya mjini Nairobi.
Agizo hilo linawahusu wanasiasa waliokuwa katika
nafasi za kuteuliwa hasa mawaziri na manaibu wao, ambapo ilieleza kwamba
kwa sasa makatibu wakuu wa Wizara ndio watakaoendesha shughuli zote
hadi mawaziri wapya watakapotangazwa rasmi.
Taarifa hiyo ilitolewa katika siku ya kwanza ya
Kenyatta ofisini akiwa mkuu wa nchi, pamoja na msaidizi wake, Ruto,
ambapo walikuwa wakipokea taarifa kutoka kwa wakuu wa usalama, maofisa
wa Serikali, mwelekeo wa maandalizi ya bajeti na kupitia kwa mara ya
mwisho namna ya muundo wa serikali wanayoihitaji.
No comments:
Post a Comment