MWANAUME
mmoja aliyemuunguza mkewe usoni kwa kutumia pasi ya umeme mjini
Singida, Baltazar Mushi a.k.a Sammayuni (33), amefikishwa mahakamani
mjini Singida kujibu shitaka la kujeruhi mkewe, Lucy Msuya(30), mwishoni
mwa wiki iliopita.
Mbele ya hakimu
Asha Mwetindwa, imedaiwa na mwendesha mashitaka inspekta msaidizi wa
polisi Shukurani Magafu kuwa, mshitakiwa amefanya kosa hilo usiku wa
februari saba mwaka huu, katika eneo la Ipembe Tarafa ya Mungumaji,
mjini Singida.
Hata hivyo
hakimu Mwetindwa amesema dhamana ipo wazi kwa mshitakiwa, kwa wadhamini
wawili ambao kila mmoja awe na Sh. Milioni tano na shauri hilo litatajwa
tena mahakamani hapo februari 25, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment