Advertise here

Monday, February 04, 2013

TUME YA KUKUSANYA NA KURATIBU MAONI YA KATIBA YAMALIZA HATUA ZA MSINGI

Tume ya kukusanya na kuratibu Maoni ya Katiba nchini imesema imemaliza hatua ya msingi ya kukusanya na kuratibu maoni kutoka kwa makundi maalum na kubainisha kuwa hatua inayofuata sasa ni kuanza kwa zoezi la uchambuzi wa maoni yote yaliyokusanywa pamoja na uandishi wa rasimu ya katiba mpya.
Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu JOSEPH WARIOBA amesema kuwa uchambuzi huo unatarajiwa kufanywa na mabaraza maalum ya Katiba kuanzia June Mwaka huu, na kuongeza kuwa mabaraza hayo yatapatikana kupitia mapendekezo maalum kutoka kwa wajumbe wa Tume hiyo.
Akizungumzia uteuzi wa mabaraza hayo JAJI WAROBA amesema, tume hiyo imejipanga kuhakikisha watu watakaopatikana kuunda mabaraza hayo wanakuwa makini, na ambao watasimamia zoezi hilo haraka na kwa umakini zaidi ili kupata katiba itakayokuwa na tija kwa Watanzania.

No comments: